Nashindwa kuelewa!

@1st Sept 2011

Nashindwa kuelewa kama serikali ya CCM hapo mwanzoni ilikuwa na nia ya kuanzisha mahakama ya Kadhi hadi pale viongozi na asasi za "kanisa" walipokuja juu dhidi yake na kupelekea kutikiswa kwa mtaji wake katika soko la kura, iweje leo tujidanganye kuwa uamuzi wa serikali haukushawishiwa ama kushuritishwa na kanisa!

Lakini pia wakati naamini katika busara za kukubali hoja hii kwa maslahi ya utanzania wetu, nashindwa kuelewa hii hoja ya kuwa kodi ya mtanzania haiwezi kutumika kuendesha mahakama ya Kadhi.

Iweje isiwe sawa kutoa kodi hizo kwa asasi za dini wakati tayari tumekuwa na tunaendelea kufanya hilo kwa kusaidia mabilioni ya kodi hizo kwa asasi na mashirika ya kidini?

Nimewahi kusikia kuwa mara baada ya Rais kushinda uchaguzi ambao inaaminika kuwa uliathiriwa na msimamo hasi wa "kanisa" dhidi ya serikali na CCM, serikali imeahidi ama kutoa zaidi ya shilingi bilioni 50 kwa mashirika na asasi kadhaa za "kanisa".

Nashindwa pia kuelewa ni vipi kodi ya mtanzania haipo kwa ajili ya maslahi ya watanzania wakati waislamu ni sehemu ya watanzania?

Na pia ni utanzania gani tunaoujenga kwa kudai kuwa ni haramu kwa kodi ya David kutumika kwa maslahi ya Omar?

Naamini kuwa msimamo huu unaweza kuwa hafueni ama ushindi kwa mtizamo wa watanzania wa upande mmoja lakini kuongeza malalamiko na hisia hasi upande mwengine. Lakini pia ni muhimu kutambua kuwa wakati wale wa upande mmoja wanadhani kuwa hotuba hii ya Rais imeonyesha uthabiti ambao wengi tunapenda kuuona unaongoza asasi hii nyeti ya Uongozi, wapo wa upande mwengine ambao watachukulia hotuba hii kama ulegelege wa kukubali kushindwa na nguvu za upande mwengine na sio kwa busara za kulinda utaifa wetu.

Ukweli ni kuwa mzizi wa tatizo hili ni ujanjaujanja uliotumika kuliingiza suala hili la mahakama ya Kadhi katika ilani ya CCM ambayo ililenga kuidhibiti CUF katika soko la kura.

Na sasa nahofia msimamo wa sasa wa serikali ya CCM ni kujaribu kuidhibiti CHADEMA katika soko la kura la 2015.

Ni wazi pia kuwa ubinafsi na ujanjaujanja wa baadhi ya wanasiasa, wasomi na zaidi viongozi wa dini ulifanikiwa katika kubomoa hoja hii ya mahakama ya kadhi na kuijengea mazingira ya uadui kati yetu badala ya kuijenga kama chachu ya upendo kati yetu.

Hii imetokana na hulka ya ushindani na propaganda hasi iliyogubika mjadala mzima wa mahakama ya Kadhi kama ilivyokuwa ukiendelea bungeni, katika vyombo vya habari, katika kampeni, misikitini na makanisani, vijiweni na hata majumbani mwetu.

Wakati waislamu waliongea kwa mtazamo wa haki yao na hisia za kubaguliwa na mfumo, wakristo walijikita zaidi "ubaya" na nia mbaya ya Mahakama ya Kadhi.

Wengi wao walikwepa kuongelea yaliyomo katika mchakato mswada wa sheria ya kuendesha mhakama hiyo na sehemu ya katiba katika suala hilo.

Kwa mtazamo wangu hutuba hii ni kipenga cha kuanzisha rasmu mjadala huu na sio kuhitimishwa.

Mwisho naamini kuwa hii ni sehemu ya changamoto ambazo kama taifa linaloendela tumekuwa na tunapaswa kupitia ili kukomaa kidemokrasia.

Muhimu ni kuendeleza utamaduni wa shauku ya kutaka kujua mambo kwa undani wake zaidi ya propaganda za viongozi wawe wa kisiasa ama kijamii na wajenga maoni wetu, kuvumiliana na pengine kuaminiana kwamba wote tuna nianjema katika kujenga tanzanianjema.

Africas silent anger!

August 2011

Reports of Libya rebels massacre of black skinned Libyans and emigrants from sub sahara Africa makes my blood boils with anger.

However this is not news to me as I saw it from the beginning that religious fanatism and racism is fundamentally centered within the NATO supported rebels.

They hated to be led by a Bedouin Ghadafi, they hated his African agenda as it was obvious during the massacre of black Africans some years ago around Benghazi and bengazis dominated eastern tripoli.

Unfortunately there those misguided Activists have guts to question why most of African government stand of not rushing to legitimize these racist fanatic myopic opportunists western nurtured and aided venture....aghhhh

Thinking Africans wont embrace rebels due to so called Ghadafi bankrolling history is as closed minded as those thinking that #libya is only oil issue.

If it's the issue of bankrolling it is the African leaders silence on the utterly abuse of their little trust to international community safeguarding their masters paycheck that should be noticed.

Actually most if those who were really bankrolled like Senegal, Gambia, Malawi and others were the first to betray him.

It's time for those who think they know us better than ourselves to understand that though we are fucked up as a continent we still cling to principles over opportunism when it comes to what is Africa and our grand aspirations!

I wish those #libya rebels cheerleaders would notice the silence anger that is boiling inside African population and how it gonna blow!