CCM bado ipo ipo!!

04/4/2012

Mnamo tarehe 1 Aprili 2012 wakati kukiwa na fununu kuwa CHADEMA inaelekea kushinda katika uchaguzi mdogo katika jimbo la Arumeru Mashiriki ambapo CHADEMA iliwakilishwa na Nasari na CCM iliwakilishwa na mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo ambaye pia ni Mkwe wa Lowassa, Sioi Sumari, nilisema kuwa Ushindi huo wa CHADEMA unapaswa kushangiliwa na wana CCM-asilia kwa kuwa ni baraka iliyojificha kwa chama chao na taifa kwa ujumla. Ninaposema CCM asilia nina maana ya wale wanaCCM ambao wanaamini katika aina ya CCM inayofuata dira ya Mwalimu Nyerere na kuamini katika matakwa ya watanzania walio wengi katika kulinda na kutetea UTU wa mtanzania.

Hawa ni wana CCM ambao kwa dhati kabisa wanaumizwa na hali ya cham chao kisera, kiitikadi na kiutendaji lakini wameamua ama wanalazimika kujikalia pembeni na kunung’unika tu wakisubiri kudura za mungu kuiokoa chama chao na pia hatima ya taifa lao;

Hapa chini ni ufafanuzi wa mtazamo wangu huo kama nilivyo ombwa na dada Jokate Mwegelo;

  1. Ushindi wa Chadema ni kushindwa kwa kundi la lowassa lilokuwa likiamini hii ni nafasi ya kuonyesha nguvu zake (nguvu za pesa). 
  2. Kushindwa kwa Lowassa ni muendelezo wa viashiria kadhaa vya hivi karibuni ikiwemo kukatwa majina ya watu wake waliokua wakitaka kugombea ubunge wa EAC na hii inapunguza myth ya kuwa ni rais mtarajiwa hivyo watu wake wengi wataanza kumkimbia na kupunguza "nguvu zake"/mgawanyiko ndani ya CCM.
  3. Kushindwa kwa CCM Arumeru kunajenga picha kuwa kuanguka kwake ni kitu kinachowezekana hivyo hii inakuwa kama kichocheo cha umuhimu wa mabadiliko ndani ya CCM na pia kuongeza idadi na nguvu ya wanamabadiliko dhidi ya wahafidhina wanaoendelea kuamini ktk nguvu ya fedha na dola.
  4. Pia Ukichukulia kuwa CCM imekuwa tayari kubadilika kila waonapo dalili ya kupoteza nafasi ya utawala ni wazi speed ya mabadiliko ya lazima itaongezeka.

Lakini pia kwa wanaoamini kuwa Ushindi wa CHADEMA kule Arumeru Mashariki ni ishara kuwa mwisho wa CCM umekaribia ni muhimu kujiuliza masuala yafuatayo kabla kuanza kuandika kumbubukizi la CCM kwa sasa, 

  • Je hii ni mara ya kwanza CCM kushindwa uchaguzi mdogo?
  • Je CHADEMA kushinda kanda ya Kaskazini ni maajabu?
  • Je mhemuko huu wa kisiasa tunaoshuhudia baadaya ushindi huu inazidi ya enzi za Mrema?
  • Na kama hakukuwa nia ya kutumia uchaguzi huu kummaliza Lowassa unadhani CCM wangeshindwa kilinda kura zao 6000? 

Ukweli ni kuwa CHADEMA inakuwa kwa kasi na ni wazi kuwa kuna kila uwezekano wa chama hiki kuweza kuondoa ukiritimba wa theluthi tatu za uwakilishi wa CCM katika bunge itakapofika uchaguzi ujao. Lakini hadi sasa naweza sema kuwa ingawa mchakato wa CCM wa 2005 uliohitimishwa pale CHIMWAGA ndio ulikuwa mwanzo wa safari yake ya mwisho, safari hiyo inaendelea lakini haijawadia katika hatima yake na CCM bado ipo ipo kwa miaka mingine mbeleni kama chama tawala…