Ya CUF cum UAMSHO na propaganda zao dhidi ya Muungano

Ni wazi kuwa baadhi ya vinara wa CUF na wadau wao UAMSHO hawautaki na wanauchukia Muungano na wameamua kufanya ajenda yao kuuvunja. Katika miezi ya karibuni vinara wa kundi hili wamakumbatia mfumo wa wanachokiita Muungano wa Mkataba ambao ni wazi wamevutiwa nao kutokana na urahisi wake wa kuuvunja Muungano. Na ukweli hii ni kama strategy ya kuwaficha ukweli wafuasi wao ambao bado wanaamini katika umuhimu wa Muungano. Wamekosa uthubutu wa kusema tuvunje Muungano lakini wanatumia neno Muungano wa Mkataba kama ngozi ya kondoo juu ya chui ambaye ni kuvunja Muungano.

Wahafidhina hawa wa harakati za kurudisha Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi, wanajua wazi kuwa madai wanayoyatoa hayawezi kukubalika kwa upande wa Bara. Hivyo madai yao ya Muungano wa Mkataba na mengineyo ni ujanja wa kuwalazimu Watanganyika ndio waamue kuvunja Muungano huo na kuwafanyia kazi wao na maslahi yao ya kihafidhina. Wanjua wazi jibu la mwisho litakuwa na tuvunje Muungano ili tukutane katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kama itahitajika tukiwa kama nchi tofauti zenye maslahi tofauti yakiwemo yanayoendana na yanayopingana.

Moja ya njia wanazotumia wahafidhina hawa kuwalaghai Wazanzibari ni kuendeleza ile ndoto ya Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi ambayo ilikuwa ikivuma kutokana na kuwa kitovu cha biashara katika Afrika Mashariki na kuaminisha watu kuwa Muungano ndio umeiondolea Zanzibar nafasi hiyo. Wanasahau kuwa geopolitics ambazo ni muhimu kwa uchumi wa eneo fulani katika enzi hizo ni tofauti kabisa na sasa. Wanasahau kuwa moja ya vitu vilivyofanikisha kujenga na kuendeleza msingi wa hali hiyo ilikuwa ni biashara ya utumwa na magendo ya bidhaa mbalimbali za thamani ya juu kutoka maeneo mengine ya Afrika Mashariki, zaidi ilikuwa kutoka Tanganyika.

Biashara ya utumwa iliendelea hata wakati wa ufalme wa Waarabu wa Omani ambao serikali iliyopinduliwa na mnayotaka kuirudisha kwa mlango wa nyuma ilikuwa ni wadau wa Sultan huyo. Lakini zaidi ninacho ongela hapa ni msingi wa uchumi uliojengwa na faida kubwa ya biashara hiyo na mabaki ya kimfumo ya biashara hiyo hata baada ya kusimamishwa kwake.

Hata baada ya biashara ya utumwa kuvunjwa Waarabu na wengineo waliendelea kutumia watumwa kuneemesha shughuli zao za kiuchumi ambazo zina uhusiano wa moja kwa moja na Zanzibar ile wanayoiota na hata baadae mfumo wa mabwana na watwana uliendelea hata baada ya uhuru wa 1963 na kukatishwa ghafla na Mapinduzi ya 1964. Hivyo huwezi kuepusha uhusiano wa bishara ya Utumwa na hali ya kiuchumi na biashara kabla ya Mapinduzi na hata mafanikio mengi ya wakati wa Karume yaliendelea kutumia matunda ya uchumi uliojengwa na mtaji uliokusanywa katia biashara ya Utumwa.

Pia wanasahau kuwa mafanikio yale ya wakati ule yalikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na mfumo wa ukoloni na ubwana na utwana uliokuwepo enzi zile ambao ulitoa nafasi maalum ya Zanzibar na sehemu fulani ya Wazanzibari kiuchumi.

Haya yote na hata hili la sasa ambapo Zanzibar bado ina nafasi ya kunufaika na soko la karibia watu milioni Arobaini na Tano la Tanganyika, kamwe hayawezi kuwepo hasa baada ya kuvunja Muungano wetu. Tukivunja Muungano Zanzibar itakuwa just another sovereign country ambayo itaangaliwa kama mshindani wa kiuchumi zaidi kuliko mshirika wa Muungano. Tukivunja Muungano hata special status ambayo Zanzibar imekuwa ikipata ndani ya Muungano wa Tanzania na katika Shirikisho la Afrika Mashariki haitakuwepo.

Hivyo kwa wale wanaoamini katika kufufua ndoto ya Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi na baadaye Muungano wanapaswa kuipima ndoto yao hiyo kwa mizania ya uhalisia wa mazingira ya sasa na sio mazingira ya wakati ule. Zanzibar njema inawezekana katika mfumo wa siasa za kuaminiana na kushirikiana ndani ya Muungano na sio katika siasa za kushindana kwa visa, chuki na utengano nje ya Muungano.

Kuhusiana na suala la Zanzibar ni nchi ama sio nchi ambalo nalo limekuwa likitumika kama propaganda dhidi ya Muungano ukweli ni kuwa kisiasa Zanzibar ni nchi lakini kisheria Zanzibar si nchi na suala lolote lonalohusiana na Muungano ni lazima lifuate taratibu za Muungano. Kwa kutumia suala la OIC, maadui wa Muungano wamewadanganya na kuwaaminisha Wazanzibari kuwa Zanzibar inazuiwa kufanya chochite wakitakacho hadi wapate ridhaa ya Tanganyia. Ukweli ni kuwa hakuna suala ambalo Zanzibar wanalokataliwa kilifanya kama sio suala la Muungano na kwa masuala ya Muungano kuna vyombo vya Muungano kulishughulikia. Yawezekana wahafidhina wanaopinga Muungano wanaamini kuwa masuala ya taratibu sio sehemu ya utamaduni wa Kizanzibari lakini kama nchi lazima utaratibu ufuatwe hasa inapohusiana na mahusiano na mataifa ya nje kama lile suala la OIC ambalo naamini ni Katika mfumo ulikokuwepo ambapo masuala ya mahusiano ya kimatifa ni suala la Muungano ni Tanzania na sio Zanizbar yenye kupaswa kujiunga na shirikisho hilo linalouunganisha Waislamu na wasio Waislam katika mashirikiano ya kimaendeleo.

Lakini huu ni unafiki wa hawa wahafidhina wanaota kurudisha Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi kung'ang'ana na Zanzibar ni nchi wakati wao ndio walioshangilia (hata mimi pia) maamuzi ya kikatiba kupitia mahakama ya rufaa katika kesi ya watu wao wa CUF waliokuwa na kesi ya uhaini lakini baadae wakaona hukumu hiyo chungu pale ilipopingana na matakwa yao wapinga Muungano. Kwa muda sasa wamekuwa wakitumia ujanja wa kulaani uhalisia huo wa kuwa Zanzibar sio nchi na hata ilipotelewa ufafanuzi katika hotuba ya Rais bungeni kuwa Zanzibar ni nchi ndani ya Tanzania na na nje ya nchi katika yale masuala yasiyo ya Muungano tu, kama mbinu ya kujenga hisia kuwa ajenda zao nyingi ikiwemo ya kuvunja Muungano ni ajenda ya Kitaifa ya Wazanzibari uuku wakijua kuwa hilo sio kweli.

Kuhusu mfumo wa kiuchumi, ni kweli Zanzibar inapaswa kuwa na nafasi maalum - special status ambayo itaiwezesha kushirikiana kiuchumi na Tanganyika na sio kushindana kama ilivyo sasa. Sioni sababu nzito ya kulazimisha bidhaa zinazoingizwa kupitia Zanzibar kutozwa kodi sawa na zile zinazoingizwa kupitia Tanganyika. Kama tumeweza kuwa na special status katika mfumo wa soko la Afrika Mashariki ambako pia Zanzibar inaendelea kufaidika nao, sioni sababu ya kushindwa kufanya hivyo ndani ya Muungano wetu.

Suala la kushindanisha uchumi wa Bara na Visiwani nakubaliana nalo kuwa linahitajika kuangaliwa upya. Inawezekana kabisa kuipa Zanzibar status maalum ya kiuchumi ambayo italindwa hata katika masuala ya Muungano au Jumuiya ya Afrika Mashariki na hiyo ndio imekuwa principle inayotumika katika negotiations zote kama Tanzania inavyosisitiza. Na kwa faida ya Zanzibar ni kuwa ili uchumi wa Zanzibar kuwa na nguvu unahitaji soko kubwa na utakuwa ni uhayawani kudhani nje ya muungano Zanzibar itapata kuwa na special status ya kiuchumi bali hilo lawezekana tu ndani ya Muungano. Hili linawezekana tu tukiwa ndani ya Muungano na si vinginevyo. Muungano huu ukivunjika Zanzibar haitakuwa na leverage za kudai special status hasa katika masuala ya kiuchumi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kuhusu hii propaganda inayoaminiwa na Wazanzibari wengi eti kodi ya ya Zanzibar inakusanywa na kupelekwa Tanganyika huu ni uzandiki mwengine usio na chembe ya ukweli. Ni propaganda ambayo inaelekea kuaminiwa hata na wale ambao wamekuwa wakisambaza huku wakijua haina ukweli wowote. Ndio matokeo ya siasa za fitna hizo. Hakuna senti ya kodi inayokusanywa Zanzibar inayoenda Bara. Pesa zote zinazokusanywa na TRA Zanzibar zinabaki kwa kutumiwa huko ktk masuala ya Muungano.

Zaidi ni kuwa Kuna kiasi kingine kikubwa kinachokusanywa Tanganyika na kuletwa huko kuongezea na hapo bado haujaingiza mabilioni mengine yanayoletwa huko kinyume cha vigezo vya Muungano. Ukweli uwazi kuwa kodi inayokusanywa Zanzibar yote hubaki na kutumika katika shuguuli za Muungano za upande wa Zanzibar na kamwe haijawahi kufikia asilimia 11 ya makusanyo. Sanasana fedha zingine ambazo hukusanywa Tanganyika huongezewa kufikia ile asilimia 4.5 ya Bajeti inayopaswa kuwa ya Zanzibar.

Kuhusu dhana ya kuwa kwa sababu Bunge la Tanzania lina wabunge zaidi ya 200 kutoka upande wa Tanganyika wakati wengine 50 wanatoka Zanzibar hivyo maslahi ua Zanzibar hayawezi kulindwa katika bunge hilo ukweli ni kuwa katika Bunge hakuna suala linalohusu Muungano linalopita bila ya kuwa na baraka za three third majority ya Wabunge kutoka Zanzibar. Sasa kama unadhani nguvu za kibunge ni kuwa na Zanzibar kuwa na wabunge 300 pia inaonyesha jinsi gani mlivyokosa busara. Labda kama na ninyi mliokimbia Zanzibar na kujilipua huko ughaibuni nanyi mnatka uwakilishi bungeni. Hilo linaweza kuzungumzwa.

Kuhusu Zanzibar kuwa na Baraza lao la Mitihani kama ilivyokuwa hapo kabla na sio kutumia mitihani na mfumo wa NECTA sidhani kama hilo tatizo kubwa sana. Kama mnataka kuendeleza uyaghe katika elimu ili kujifurahisha kuwa vijana wenu wamefaulu mnaweza kuwa na baraza lenu la mitihani. Lakini muwe tayari tu kwa vijana wenu ama watosheke na nafasi za vyuo vya elimu ya juu huko Zanzibar na vyenye sifa za kutambulika kimataifa ama muwe tayari kufanya mitihani maalum ya kuweza kuingia katika vyuo vya bara na kwengineko.

Huu ujinga wa kulaumu NECTA kufeli kwa vijana wa Zanzibar ambao wenyewe mnajua walivyokosa nidhamu na tamaduni za elimu unazidi kuwadanganya vijana wa Zanzibar ambao sasa imekuwa fashion kujigamba kuwa hawajasoma na wala hawana kazi. Hata yule kijana aliyekuwa wa mwisho kabisa darasani naye sasa anaamini alifelishwa. Wanatumia sumu kupata mradi wao sasa, lakini sumu hiyohiyo ndio inaaendelea kuathiri msingi mkuu wa maendeleo ya jamii yenu, ELIMU ya vijana wenu. Kama tatizo ni NECTA mbona vijana wa Pemba na wale wenye kuishi katika mazingira ya kielimu wanafaulu?

Kuhusu umeme wa Tanesco ukweli ni kwamba Zanzibar inauziwa kwa bei tofauti na wengine. Serikali ya Muungano ina-subsidize kwa kiasi kikubwa. Lakini pia kiasi kikubwa cha deni hakilipwi na huishia kwa hazina ya Muungano kubeba mzigo wa madeni hayo. Lakini ni kweli suala hilo sio kubwa kwani uwezekano wa wafadhili kuwawekea mitambo ya gesi upo lakini suala ni kuwa na uchumi wa kuweza kuendesha mitambo hiyo na sio kuwa tegemezi jumla jumla.

Na kuhusu dai la kuwa Wazanzibari wanapaswa kuwa na paspoti yao wengine hata wakadai kurudishiwa paoti yao ambayo ukweli Zanzibar huru haijawahi kuwa nayo labda wakimaanisha ile ya Sultan wa Omani ni kweli tukifikia kuwa na paspoti tofauti Wazanzibar wataweza kwenda Tanganyika kama wageni wengine kutoka Kenya endapo mtaweza kuingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Lakini pia thamani ya passpoti inategemea na hali za kisiasa na uchumi wa nchi hiyo. Ukiangalia mbele kuna kila dalili ya Zanzibar kuwa black spot katika enzi hizi za ugaidi wa "waislamu wenye siasa kali" ambao wamejificha katika kivuli cha CUF na sasa wameanza kujitokeza kaika sura ya UAMSHO. Sasa kama Wazanzibari wako tayari kuondokana na kivuli cha Utanzania na kuingia katika kivuli cha Zanzibar ya UAMSHO na majinamizi mengine, then wanapaswa kuangalia machaguo yao kwa uangalifu zaidi.

Wadau wengi wa Ushirika wa kuvunja Muungano ndani ya CUF wanaamini ama hupenda kuwaaminisha Wazanzibari kuwa baada ya kuvunja Muungano tutaendelea kuwa na mahusiano ya kindugu kati ya Tanganyika na Zanzibar. Hili wakimaanisha kuwa Wazanzibari waliopo Tanganyika hawataathirika na biashara na maingiliano mengine ya kijamii yataendelea kuwa kama kawaida. Huu ni uongo na kama wapo wanaoamini hilo basi ni wajinga.

Ukweli ni kuwa tukivunja Muungano haki za Mzanzibari aliyepo Tanganyika zitabadilika na hatakuwa na nafasi kama aliyo nayo sasa. Atakauwa mgeni kama alivyo Mkenya ama Mganda na usitegemee kuwa Wazanzibari wataendelea kupata upendeleo ktk suala la Ardhi. Lakini pia hata wale tutakaoamua kuwa Watanganyika ni wazi tutabaguliwa zaidi na madhila ya siasa za chuki mnazoendesha ninyi huko hivi sasa zinatatuangukia. Kumbuka huku Tanganyika kuna zaidi ya Wazanzibari 300,000 wahamiaji na zaidi ya 1,000,000 ambao ni vizazi vyao ama wenye nasaba za Kizanzibari. Wengi wao ni Wapemba. Hawa wakilazimika robo tu kurudi Zanzibar sijui hizo social and economic pressures mtazihandle vipi na zaidi wakizaliana nao Zanzibar itakuwa kama Rwanda kwa kukosa ardhi ya kutosha na hivyo itaongezea chachu ya siasa za chuki miongoni mwenu na kamwe Zanzibar haitaweza kustabilize na kujiendeleza Kiuchumi.

Kuvunjika kwa Muungano lazima kutakuwa na remifications zake na hakuna mwenye kuweza kujua ama kucontrol dynamics za baada ya Muungano. CUF wengi huangalia Muungano katika mizania ya imani kuwa bila ya Muungano ni rahisi wao kuchukua utawala wa Zanzibar na ili kufikia lengo hilo kila kitu ni halali na kuwa wanauwezo wa kucontrol dynamics za baada ya hapo. Hii ni falacy ambayo haina uhalisia wowote. Dynamics za baada ya muungano hasa katika suala mahusiano ya Wazanzibari wenyewe kwa wenyewe na Wazanzibari na Watanganyika zitategemea zaidi na mchakato wa kuvunja Muungano kama unavyendelea sasa. Kama Muungano utavunjika kwa makubaliano ya pamoja ama kwa vitimbwi na chuki ambazo CUF na Wadau wao UAMSHO wanavyozipalilia hivi sasa ndio itakavyo shape dynamics za mahusiano yetu baada ya Muungano kuvunjika. Zaidi huu upatu wa CUF na UAMSHO unapelekea kufanya geopolitical calculations kati ya Tanganyika na Zanzibar nje ya Muungano kutokuwa za kidugu wala za kuaminiana.


Wapo wanaoijidanganya kuwa wanaweza kuchezea Muungano na baadae wataweza kutumia baadhi ya vyombo vya Muungano kuwasaidia kuwaepusha na majinamizi ya kuamalizana wao kwa wao. Wanajidanganya kuwa hata wakivunja Muungano bado mtaweza kutumia majeshi ya Muungano kuwa buffer kati yao msimalizane. Ujumbe ni kuwa katika harakati hizi zao za sasa ni muhimu wakajiandaa Vizuri na mpambano wa mahafidhina wa ASP MASALIA na MAZIMWI YA HIZBU peke yao kwani hakuna uhakika kuwa Watanganyika hasa baada ya kutukanwa, kulaaniwa na hata kuuawa hovyo kama hali inavyoendelea hivi sasa watakuwa tayari kujitolea muhanga huo kwa watu ambao walipokuwa pamoja hawakuonyesha kuwathamini!


Mahusiano ya Tanganyika na Zanzibar mara baada ya kuvunjika kwa Muungano pia yaategemea na Mtu ama Chama kitakachokuwa madarakani wakati huo na mara baada ya kuvunjika kwa Muungano huo. Kuna scenario moja ambayo wengi hawaiangalii. Hii ni scenario ya chama cha CUF kikitwaa madaraka Zanzibar na CHADEMA kutwaa madaraka upande wa Tanganyika. Sioni mahasimu hawa kisiasa na kijamii wanavyoweza kuwa na ustaarabu wa kuheshimiana na kudumisha historia ya udugu wetu. Wote hawa nawajua na prejudices za udini na nyinginezo miongoni mwa fikra zao kisiasa ni kubwa mno ambazo kuna uwezekano mkubwa ndizo zitakuwa zinaongoza misimamo yao kuhusiana na mahusiano ya watu wa pande zao. Kama Zanzibar ni CUF na Tanganyika ni CHADEMA, dyanamics za mahusiano yetu baada ya kuvunja Muungano zitakuwa tofauti sana. Hii ni scenario ambayo fanatics united against the Union upande wa Zanzibar wameshindwa kuiona hadi sasa ama wameamua kuidharau kutokana na kugubikwa zaidi na chuki zao na urari wao wa kurudisha enzi za kabla ya mapinduzi. Na scenario kama hii ndio inaniambia kuwa hii propaganda ya kuwaaminisha Wazanzibari kuwa mambo yatakuwa shwari tu baada ya kuvunja Muungano ni falacy ambayo ina hatari kubwa kwa maslahi ya Wazanzibari zaidi ya Watanganyika!

Ninachosema kuwa ndoto ile ya Zanzibar ile ya kabla ya Mapinduzi ni falacy kwani haiangalii mazingira ya wakati ule na inadharau kwa makusudi mazingira ya sasa! Na kusisitiza kuwa Zanzibar bado ina nafasi ya uhakika zaidi ndani ya Muungao na sio nje ya Muungano! Anyway, najua ni vigumu kurationalize na fanatics kwani kwao rationality ni jambo adimu sana lakini naamini wapo wenye upeo mkubwa wa kupima mambo ambao wataweza kuchambua masuala haya kwa utulivu zaidi kuliko hizi hisia za Ki-UAMSHO!