Kuhusu Hekaya ya wahafidhina wa CHADEMA dhidi ya ZItto

Kuna watu wengi wamekuwa wakiniuliza ... Eti kaka hii ripoti ina ukweli wowote... Kwa ni ninaowaheshimu nimewajibu kuwa hiyo ni riwaya ya kawaida ya chadema maslahi ambayo ilianza kuatengenezwa wakati uke Zitto alipojaribu kugombea uenyekiti. Nahata base ya kiasi cha fedha kinachotajwa ni kilekile ambacho wakati ule Mbowe alijaribu kuwarubuni waandishi akidai kuwa ndio alichonacho katika benki ya .... Kitu ambacho waandishi makini kama Msaki na Kibanda walikataa ujinga huo lakini ukachukuliwa na kutumiwa na Said Kubenea ambaye kuanzia wakati huo akawa mshirika wa Mbowe hadi hivi karibuni alipohamia kwa Mr Robot. Kwa wengine ambao siwathamini sana nawaambia, namshukuru Mungu kwa kuniepusha ukaribu na mtu mwenye akili fupi kama wewe ambaye unashindwa kung'amua kwa urahisi kuwa hiyo ni riwaya ya wajinga wakiwa na malengo ya kuteka akiki za wajinga kama wewe! Siwezi kuwa na rafiki anayeweza kuhadaika na riwaya ya kina Slaa na mwenza wake, nasikia siku hizi anajita bulisha kama mkewe, na vijana wao wehu kama kina Yericko, Ben Saanane na wengineo wenye chuki zao kama mtuhumiwa ugaidi Kilewo na jamaa zake wengine wanaodhani kuwa chama hicho ni chama cha nyumbani na wengine wote wanaothubutu kutishia nafasi yao huko ni maadui wa kuangamizwa. Lakini pia nafurahishwa kuwa hii vita ya akili fupi dhidi ya fikra pana imefikia kuwaibua maadui wote Zitto na sasa wanaonekana mchana kweupe kwa kujianika na siasa zao za fitna, uzandiki na chuki. Kwa wanaosema kuwa uongozi wa chama uongee, acheni kujidanganya kwani uongozi wa chama huo unahusika moja kwa moja na riwaya hii na hata kuipigania kutolewa mitandaoni....

No comments: